Tshala Muana: Malkia aliyelivutia bara la Afrika

Chanzo cha picha, Getty Images
Miongoni mwa waimbaji mashuhuri zaidi barani Afrika, Tshala Muana, ambaye alifariki wiki iliyopita akiwa na umri wa miaka 64, alijulikana pia kwa sauti yake ya kusisimua na kucheza kwa kuvutia kimapenzi ambayo ilisababisha ghasia na kutaka apigwe marufuku.
Hatua hizo hazikufua dafu kwa kuwa watu wengi walitaka kumuona akicheza na alikuwa na umaarufu mkubwa.
Alisemekana kuwa na mahusiano ya kimapenzi na baadhi ya viongozi wa Afrika na hata kuimba kuhusu rais ambaye hakutajwa jina ambaye alijaribu sana kuwa na mahusiano naye ya kimapenzi.
Lakini alianza maisha ya uimbaji na akiwa na umri wa miaka 22 aliondoka nchini kwake - wakati huo Zaire, ambayo sasa ni Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo - ili kufuata ndoto yake ya kuwa mwimbaji na dansi. Aliporejea miaka sita baadaye mwaka wa 1986, alikuwa kila kitu alichotamani kuwa - Malkia wa Mutuashi, ambaye sauti zake ziliyeyusha sauti barani Afrika na kwingineko.
Aliondoka tena Jumamosi, 10 Desemba, Wakati huu hakutueleza kuwa anaenda kuvuka Mto baridi wa Kongo ili kuelekea Afrika Magharibi. Aliondoka kwa amani, milele.
"Kwaheri dada yangu mdogo Elisabeth Tshala Muana," Dino Vangu, ambaye alifanya kazi na nyota huyo katika albamu yake ya 1989 ya Biduayi, alichapisha kwenye Facebook.
"Hii ni kazi kubwa na nzuri zaidi katika kazi zangu zote, utukufu wote ni kwa Mungu," alisema Souzy Kasseya, mpiga gitaa anayesifika kwa kuibua kipaji cha Tshala Muana.
Katika zaidi ya miongo mitatu kati ya kuondoka kwa Muana kwa mara ya kwanza kutoka DR Congo na kifo chake, alivutia watazamaji, na kusaidia kuinua hadhi ya lugha yake ya asili ya Tshiluba na ngoma yake ya kitamaduni, Mutuashi.
"Ninapenda ukweli kwamba alibaki kwenye mstari wake, akiimba kwa lugha yake ya asili na kukuza rhuba yake ya asili na utamaduni wake. Hii ilikuwa ya kipekee sana," alisema msanii wa reggae kutoka Uganda Tshaka Mayanja.

Chanzo cha picha, Getty Images
Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.
Bonyeza hapa kujiunga
Mwisho wa Whatsapp
Wanamuziki wa Kongo ambao walitawala vituo vya redio na vilabu vya usiku kote barani Afrika kwa miaka mingi - hadi kuibuka kwa Afrobeats - wengi wao walirekodi rhumba, muziki wenye asili ya nchini Cuba. Walitumia gitaa zenye kumeta-meta na kuimba katika Kilingala, lugha ya jiji kuu, Kinshasa, au Kifaransa.
Lakini Muana alitembea hatua zake mwenyewe, karibu peke yake. Akiimba katika Tshiluba na kucheza Mutuashi, alitoa sauti kali zilizokita mizizi katika nyimbo za kitamaduni, lakini alitumia ala za kisasa ambazo ziliwapa sauti zaidi. Ilibidi ashawishiwe kuimba kwa lugha ya mama.
"Ni mpangaji wake Kasseya ndiye aliyemshawishi kutumia Tshiluba kama mtindo wa kipekee," alisema Djouna Mumbafu, mwimbaji na mchezaji ambaye aliwahi kutumbuiza na kundi maarufu la Kikongo, Empire Bakuba, linaloongozwa na nyota Pépé Kallé.
Inavyoonekana, Kasseya alikuwa ameona vya kutosha kwa Muana wakati anajifunza na kusadikishwa kwamba alikuwa na ujasiri zaidi akiimba Tshiluba na kucheza Mutuashi.
Hata hivyo, Muana aliimba kwa Kilingala pia, kwa mfano katika wimbo wa Nasi Nabali (Nimeolewa), ambapo anasimulia jinsi ndoa inavyomletea mwanamke heshima na kuwazuia wanaume kuwadhalilisha.
Mwimbaji huyo aliyejitengeneza, kuwa mcheza muziki, muimbaji na mwandishi wa nyimbo alikua mmoja wa wanamuziki wa kike maarufu kutoka Afrika. Kuanzia Senegal hadi Kenya, maonesho ya Muana yaliuzwa wakati wa enzi yake, kuanzia 1986 hadi mwisho wa milenia. Alizua ghasia kiasi kwamba, mnamo mwaka 1992 nchini Zambia, mabomu ya machozi yalirushwa kudhibiti watazamaji.
Mutuashi awali lilikuwa neno la Tshiluba, sauti ya kutia moyo kwa wachezaji kucheza kwa nguvu zaidi, Muana aliwahi kufafaua.
Neno hilo hatimaye likawa sawa na aina ya uchezaji wa Muana mwenyewe. Papy Tex Matolu, ambaye alianzisha Empire Bakuba pamoja na Pépé Kallé, alisema Mutuashi imekuwa sehemu ya muziki wa kitamaduni wa Kongo tangu enzi za kale.
"Tshala Muana ameeneza tu sehemu hii ya utamaduni wetu wa Kasaian kwa hadhira ya kimataifa," alisema. Mutuashi ni ngoma ya kitamaduni ya watu wa Luba kutoka eneo la kati la Kasai nchini DR Congo.
Wakiwa wamevaa kanga kuzunguka makalio ili kusisitiza mwendo wa ngoma, Waluba wangecheza kinyama kama vile wanaita miungu ya uzazi. Ilichezwa kusherehekea kuzaliwa kwa mtoto, haswa mapacha.
Kwa kuongezeka kwake, Muana aligeuza umbo la densi kwenye makalio yake, halisi. Racy alidharauliwa kwenye matamasha yake. Angetokea akiwa amevalia gauni la kifundo cha mguu lenye mpasuko hadi kiunoni.
Wacheza-dansi wake wangekuwa kimahaba zaidi, wakifunika sehemu kidogo ya mwili na matiti yao tu. Kisha wangecheza kwa njia ambazo ziliwafanya watazamaji kupata mizuka - wanaume na wanawake. Walakini, haikuwa nzuri kila wakati. Mutuashi ilichukiwa na wengi. Nchini Zambia mwaka wa 1992, Mchungaji Stan Kristafor, waziri wa habari, alijaribu kumpiga marufuku Muana kwa sababu uchezaji wake na uvaaji ulikuwa "unaovutia sana mapenzi".
Alikataliwa na bunge, na Muana alitumbuiza katika maonesho yaliyouzwa sana ambapo yalisababisha CD iliyotayarishwa hasa kwa hadhira ya Zambia. Nchini Uganda mwaka 2009, alitetea mavazi hayo kama ya "utamaduni".
"Tunaifanya kuwa ya kisasa kidogo na hatuwezi kuondoa asili ya Mutuashi. Ni utambulisho wa watu wa kabila la Kasai," aliwaambia wanahabari.












