AFCON 2025: Tanzania yaweka historia, yatinga 16 bora

Chanzo cha picha, Getty Images
Tanzania imeandika historia mpya kwenye michuano ya AFCON 2025 baada ya kufuzu hatua ya 16 bora kupitia nafasi ya timu bora zilizomaliza nafasi ya tatu, hatua iliyothibitisha kuwa safari ya Taifa Stars kwenye mashindano haya haikuwa ya kushiriki tu bali ya kushindana.
Katika historia ya AFCON, njia hii ya kufuzu si jambo geni kwa mataifa yaliyokuja kufanya makubwa. Benin, kwa mfano, waliwahi kufika hadi robo fainali mwaka 2019 licha ya kutoshinda mchezo hata mmoja kwenye hatua ya makundi.
Vilevile, Ivory Coast, mabingwa watetezi wa sasa, walipitia njia kama ya Tanzania kufuzu kama 'best losers', nafasi ya tatu kabla ya kuibuka mabingwa, jambo linaloonyesha kuwa nafasi hii si ya bahati bali ni fursa halali ya kujijenga na kusonga mbele.
'Sikutarajia kwamba ingefuzu 16 bora, ni hatua kubwa", anasema Amri Kiemba, nyota wa zamani wa Tanzania na mchambuzi wa soka.
Kwa Tanzania, kufuzu huku kunapata uzito zaidi kutokana na ukweli kwamba imefunga katika kila mchezo wa kundi, ikikusanya mabao matatu dhidi ya Nigeria, Uganda na Tunisia. Hii ni ishara ya maendeleo ya wazi, hasa ikizingatiwa kuwa Taifa Stars kwa muda mrefu ilihangaika kupata mabao kwenye mashindano makubwa.
Mchango wa kocha Miguel Gamondi hauwezi kupuuzwa. Kocha huyo ameonyesha uwezo wa kusoma mechi, kubadilisha mifumo ndani ya mchezo na kuipa timu uthubutu wa kucheza bila woga dhidi ya wapinzani wakubwa.
Chini yake, Tanzania imeonekana kuwa timu yenye mpangilio, nidhamu ya kiufundi na imani ya kushindana hadi dakika ya mwisho sifa ambazo hazikuwa za kawaida kwa Taifa Stars kwenye AFCON zilizopita.
Gamondi ameweza pia kuimarisha utambulisho wa timu, akichanganya wachezaji wa ndani na wa nje kwa uwiano mzuri, huku akiwapa majukumu yanayoendana na uwezo wao. Matokeo yake ni Tanzania ambayo haijafungwa kirahisi, inashambulia kwa mpango na inalinda matokeo kwa umakini mkubwa.
Katika hatua ya 16 bora Tanzania itakutana na kigogo na mwenyeji, Morocco, mchezo utakaopigwa Januari 4, 2026. Historia inaonyesha kuwa timu zilizopita kwa mlango huu zimeweza kuandika simulizi kubwa zaidi. Kwa Taifa Stars, ujumbe umefika wazi kwamba ndoto bado hai.
Timu zilizofuzu 16 bora
Morocco
🇲🇱 Mali
🇪🇬 Egypt
🇿🇦 South Africa
🇳🇬 Nigeria
🇹🇳 Tunisia
🇹🇿 Tanzania
🇸🇳 Senegal
🇨🇩 Congo DR
🇧🇯 Benin
🇩🇿 Algeria
🇧🇫 Burkina Faso
🇸🇩 Sudan
🇨🇮 Ivory Coast
🇨🇲 Cameroon
🇲🇿 Msumbiji
Kombe la Mataifa ya Afrika 2025
- P - Imecheza
- W - Imeshinda
- L - Imeshindwa
- D - Imetoka Sare
- GD - Tofauti ya bao
- Pts - Alama
-
-
Kundi A
Nchi P W L D GD Pts Morocco 3 2 0 1 5 7 Mali 3 0 0 3 0 3 Comoros 3 0 1 2 -2 2 Zambia 3 0 1 2 -3 2 -
21/12/2025, 19:00Morocco 2-0 Comoros-(Penati)(Uwanja wa Prince Moulay Abdallah)
-
22/12/2025, 14:00Mali 1-1 Zambia-(Penati)(Uwanja wa Mohamed V)
-
26/12/2025, 17:30Zambia 0-0 Comoros-(Penati)(Uwanja wa Mohamed V)
-
26/12/2025, 20:00Morocco 1-1 Mali-(Penati)(Uwanja wa Prince Moulay Abdallah)
-
29/12/2025, 19:00Comoros 0-0 Mali-(Penati)(Uwanja wa Mohamed V)
-
29/12/2025, 19:00Zambia 0-3 Morocco-(Penati)(Uwanja wa Prince Moulay Abdallah)
-
-
Kundi B
Nchi P W L D GD Pts Misri 3 2 0 1 2 7 Afrika Kusini 3 2 1 0 1 6 Angola 3 0 1 2 -1 2 Zimbabwe 3 0 2 1 -2 1 -
22/12/2025, 17:00Afrika Kusini 2-1 Angola-(Penati)(Uwanja wa Marrakech)
-
22/12/2025, 20:00Misri 2-1 Zimbabwe-(Penati)(Uwanja wa d' Agadir)
-
26/12/2025, 12:30Angola 1-1 Zimbabwe-(Penati)(Uwanja wa Marrakech)
-
26/12/2025, 15:00Misri 1-0 Afrika Kusini-(Penati)(Uwanja wa d' Agadir)
-
29/12/2025, 16:00Angola 0-0 Misri-(Penati)(Uwanja wa d' Agadir)
-
29/12/2025, 16:00Zimbabwe 2-3 Afrika Kusini-(Penati)(Uwanja wa Marrakech)
-
-
-
-
Kundi C
Nchi P W L D GD Pts Nigeria 3 3 0 0 4 9 Tunisia 3 1 1 1 1 4 Tanzania 3 0 1 2 -1 2 Uganda 3 0 2 1 -4 1 -
23/12/2025, 17:30Nigeria 2-1 Tanzania-(Penati)(Uwanja wa Fès)
-
23/12/2025, 20:00Tunisia 3-1 Uganda-(Penati)(Uwanja wa Rabat)
-
27/12/2025, 17:30Uganda 1-1 Tanzania-(Penati)(Uwanja wa El Barid)
-
27/12/2025, 20:00Nigeria 3-2 Tunisia-(Penati)(Uwanja wa Fès)
-
30/12/2025, 16:00Tanzania 1-1 Tunisia-(Penati)(Uwanja wa Rabat)
-
30/12/2025, 16:00Uganda 1-3 Nigeria-(Penati)(Uwanja wa Fès)
-
-
Kundi D
Nchi P W L D GD Pts Senegal 3 2 0 1 6 7 DR Congo 3 2 0 1 4 7 Benin 3 1 2 0 -3 3 Botswana 3 0 3 0 -7 0 -
23/12/2025, 12:30DR Congo 1-0 Benin-(Penati)(Uwanja wa El Barid)
-
23/12/2025, 15:00Senegal 3-0 Botswana-(Penati)(Uwanja wa Tanger)
-
27/12/2025, 12:30Benin 1-0 Botswana-(Penati)(Uwanja wa Rabat)
-
27/12/2025, 15:00Senegal 1-1 DR Congo-(Penati)(Uwanja wa Tanger)
-
30/12/2025, 19:00Benin 0-3 Senegal-(Penati)(Uwanja wa Tanger)
-
30/12/2025, 19:00Botswana 0-3 DR Congo-(Penati)(Uwanja wa El Barid)
-
-
-
-
Kundi E
Nchi P W L D GD Pts Algeria 3 3 0 0 6 9 Burkina Faso 3 2 1 0 2 6 Sudan 3 1 2 0 -4 3 Equatorial Guinea 3 0 3 0 -4 0 -
24/12/2025, 12:30Burkina Faso 2-1 Equatorial Guinea-(Penati)(Uwanja wa Mohamed V)
-
24/12/2025, 15:00Algeria 3-0 Sudan-(Penati)(Uwanja wa Prince Moulay El Hassan)
-
28/12/2025, 15:00Equatorial Guinea 0-1 Sudan-(Penati)(Uwanja wa Mohamed V)
-
28/12/2025, 17:30Algeria 1-0 Burkina Faso-(Penati)(Uwanja wa Prince Moulay El Hassan)
-
31/12/2025, 16:00Equatorial Guinea 1-3 Algeria-(Penati)(Uwanja wa Prince Moulay El Hassan)
-
31/12/2025, 16:00Sudan 0-2 Burkina Faso-(Penati)(Uwanja wa Mohamed V)
-
-
Kundi F
Nchi P W L D GD Pts Ivory Coast 3 2 0 1 2 7 Cameroon 3 2 0 1 2 7 Msumbiji 3 1 2 0 -1 3 Gabon 3 0 3 0 -3 0 -
24/12/2025, 17:30Ivory Coast 1-0 Msumbiji-(Penati)(Uwanja wa Marrakech)
-
24/12/2025, 20:00Cameroon 1-0 Gabon-(Penati)(Uwanja wa d' Agadir)
-
28/12/2025, 12:30Gabon 2-3 Msumbiji-(Penati)(Uwanja wa d' Agadir)
-
28/12/2025, 20:00Ivory Coast 1-1 Cameroon-(Penati)(Uwanja wa Marrakech)
-
31/12/2025, 19:00Gabon 2-3 Ivory Coast-(Penati)(Uwanja wa Marrakech)
-
31/12/2025, 19:00Msumbiji 1-2 Cameroon-(Penati)(Uwanja wa d' Agadir)
-
-
-
Hatua ya 16 Bora
-
03/01/2026, 16:00Senegal 3-1 Sudan-(Penati)(Uwanja wa Tanger)
-
03/01/2026, 19:00Mali 1-1 Tunisia-(Penati)(Uwanja wa Mohamed V)
-
04/01/2026, 16:00Morocco 1-0 Tanzania-(Penati)(Uwanja wa Prince Moulay Abdallah)
-
04/01/2026, 19:00Afrika Kusini 1-2 Cameroon-(Penati)(Uwanja wa El Barid)
-
05/01/2026, 16:00Misri 3-1 Benin-(Penati)(Uwanja wa d' Agadir)
-
05/01/2026, 19:00Nigeria 4-0 Msumbiji-(Penati)(Uwanja wa Fès)
-
06/01/2026, 16:00Algeria 1-0 DR Congo-(Penati)(Uwanja wa Prince Moulay El Hassan)
-
06/01/2026, 19:00Ivory Coast 3-0 Burkina Faso-(Penati)(Uwanja wa Marrakech)
-
-
Robo- Fainali
-
09/01/2026, 16:00Mali 0-1 Senegal-(Penati)(Uwanja wa Tanger)
-
09/01/2026, 19:00Cameroon 0-2 Morocco-(Penati)(Uwanja wa Prince Moulay Abdallah)
-
10/01/2026, 16:00Algeria 0-2 Nigeria-(Penati)(Uwanja wa Marrakech)
-
10/01/2026, 19:00Misri 3-2 Ivory Coast-(Penati)(Uwanja wa d' Agadir)
-
-
Nusu- Fainali
-
14/01/2026, 17:00Senegal 1-0 Misri-(Penati)(Uwanja wa Tanger)
-
14/01/2026, 20:00Nigeria 0-0 Morocco-(Penati)(Uwanja wa Prince Moulay Abdallah)
-
-
Nafasi ya 3 na ya 4
-
17/01/2026, 16:00Misri 0-0 Nigeria-(Penati)(Uwanja wa Mohamed V)
-
-
Fainali
-
18/01/2026, 19:00Senegal 1-0 Morocco-(Penati)(Uwanja wa Prince Moulay Abdallah)
-













