Meli katika bahari hindi hupata matatizo makubwa katika eneo hili, kwanini?

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Meli katika eneo hili hupata matatizo makubwa

Je unalijua eneo lenye kina kirefu zaidi duniani? Basi lipo katika bahari hindi.

Mvuto duniani katika eneo hili ni wa kiwango cha chini. Kwanini iwe hivyo? Watafiti wawili kutoka India walijibu kitendawili hiki.

Kama tulivyojifunza shule , duniani ni mzunguko,. Kasi ya mvuto wad unia ni mita 9.8 kwa sekundę moja.

Uzito wa ardhi ya dunia yetu ilio umbo la viazi hutofautiana kulingana na eneo. Hutegemea na uzito wa eneo hilo.

Maeneo mengine yanaweza kuwa na mvuto wa chini au wa juu kuliko wastani.

.

Chanzo cha picha, THAT

Je, vitu huanguka kwenye shimo la mvuto?

Tunapozungumzia mambo haya ni muhimu tukaelewa 'shimo la mvuto'.

Katika hatua hii ya kina kuna tofauti kubwa zaidi katika mvuto.

"Ni mahali muhimu zaidi Duniani," anasema Gabriela Fernández Viejo wa Chuo Kikuu cha Oviedo, ambaye ana PhD katika jiografia.

Hatahivyo, inasemekana kwamba vitu havianguka ndani yake kama shimo la kawaida au bonde. Wanasema shimo hili halionekani.

Meli ambazo zilisafiri huko miongo kadhaa iliyopita zilikuwa na tukio la kushangaza mahali hapa. Wanagundua mabadiliko katika mvuto katika eneo hilo. Baadaye satelaiti zilithibitisha hilo.

Lakini, hawakuweza kujua sababu ya shimo hilo ardhini. Hata hivyo, sasa baadhi ya maelezo yanapatikana kuhusu hili.

.

Chanzo cha picha, THAT

Maelezo ya picha, Ramani inayoonyesha eneo la shimo la mvuto

Shimo la kilomita 30 mraba

Shimo hili liko mita 105 chini ya uso wa bahari.

Eneo lake ni kilomita za mraba laki 30. Hii inaitwa Sheria ya Geoid ya Bahari ya Hindi (IOGL).

Mvuto wa chini kabisa Duniani uligunduliwa hapa.

Tulifundishwa shuleni kwamba ambapo kuna uzito mdogo, kuna mvuto mdogo.

Shimo hili katika Bahari ya Hindi lina mvuto wa chini kabisa. Lakini, kwa nini hivyo?

Wanajiolojia wanatoa maelezo tofauti kwa hili.

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Hatari kubwa ya moto'

"Nadharia tulizo nazo ni kwamba wakati sahani mbili za bara zinapogongana, moja yao inasukuma nyingine chini, ambayo hupunguza uzito wake," Fernandez alisema.

Kulingana na watafiti, shimo hili liliundwa wakati bara la kale la Gondwana na bara la Laurasia lilipogongana miaka milioni 25 iliyopita. Baada ya hapo ikawa Bahari ya Hindi. Lakini, maelezo haya hayakuwa ya kuridhisha kwa watafiti walioona mabadiliko ya anga katika Bahari ya Hindi.

Hata hivyo, Dipanjan Pal na Atrei Ghosh wa Taasisi ya Sayansi ya India wametoa maelezo tofauti.

Kwa ajili hiyo, waliunda mifano 19 ya utabiri wa kijiolojia kwa usaidizi wa kompyuta juu ya mabadiliko ambayo yametokea duniani kwa miaka milioni 14 iliyopita.

Mambo kama vile nguvu ya uvutano kwenye uso wa Dunia, halijoto, na muda unaochukua kwa mabamba ya bara kutengana huzingatiwa.

Kwa hivyo sampuli sita kati ya 19 zilizowasilishwa na wawili hao zilionekana kisayansi.

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya watafiti wa Kihindi

Ufafanuzi wa watafiti hao wa India pia unathibitisha kuwa Bahari ya Hindi iliundwa kutokana na kujitenga kwa Bara la India na Bara la Gondwana. Ikiwa hiyo ni kweli, vipi kuhusu Afrika?

Bahari ya Tethys yenye baridi kali ilielekea Afrika Mashariki, ambako iligongana na uji wa magma wenye moto mkali chini. Kulingana na Fernandez ulikuwa moto mkubwa zaidi wakati huo.

Mtetemo mkubwa hutokea wakati sehemu za moto na baridi zinapogongana. Tukio hili lilisababisha uundaji mkubwa wa kijiolojia. Ni kwa sababu hii kwamba sehemu ya Bahari ya Hindi ina msongamano mdogo na mvuto mdogo, kulingana na ripoti ya watafiti wa India.

Kulingana na Fernandes maelezo haya yanafaa zaidi. Kwa sababu ni uchanganuzi unaozingatia historia ya kijiolojia, data ya hisabati na miundo ya kompyuta ya kijiolojia.