Mabadiliko ya tabianchi yanavyoathiri ladha ya bia

Chanzo cha picha, Getty Images
Bia, ni kinywaji kinachogusa hisia zetu. Lakini, kadiri dunia inavyoshuhudia mabadiliko ya tabianchi, ndivyo ladha ya bia, mojawapo ya vinywaji maarufu duniani, inavyoweza kubadilika pia.
Kwa ladha yake ya kutosheleza na kuburudisha, ni vigumu kupata kinywaji kinachovutia kama bia iliyojaa. "Sio tamu wala chungu pekee, taratibu huvutia kunywa zaidi na zaidi,na hiyo ni sifa ngumu kuelezea," anasema Mirek Trnka, mtafiti kutoka Chuo Global Change Research Institute cha Jamhuri ya Czech.
Ladha ya bia inatengenezwa na mchanganyiko wa vimelea vya kemikali kutoka kenye malighafi tatu: 'Hops' maua ya kike pekee ambayo hutumika katika kutengeneza bia, hamira inayotumika kuchachusha bia, na shayiri.
Lakini sasa, mabadiliko ya tabianchi yanatishia uzalishaji wa vimelea viwili kati ya hivi – shayiri na hops. Trnka na wenzake wanasema kwamba mazao ya kiasili ambayo wazalishaji bia wanategemea kutengeneza bia – yanayoitwa hops za kiasili – yatakabiliwa na "ugumu zaidi kulima."
Utafiti wa Trnka unaonyesha kwamba uzalishaji wa maua au hops za kiasili umepungua kwa asilimia 20 tangu miaka ya 1970 katika baadhi ya maeneo makubwa yanayozalisha zao hilo barani Ulaya.
Utafiti wa Trnka unahitimisha kwamba viwango vya asidi vitapungua kwa asilimia 31 ifikapo mwaka 2050.
Je, bia inakutana na janga la kimapokeo? Je, nini kinachoweza kufanyika ili kuhifadhi ladha yake katika siku zijazo?
Bia, mojawapo ya vinywaji vinavyopendwa duniani, na kinywaji cha kileo kinachopendwa zaidi kwa kiasi, kimekuwa sehemu ya jamii tangu wanadamu walipogundua kilimo.
Ushahidi wa vinywaji vya pombe vilivyotengenezwa kutokana na nafaka vimepatikana kutoka maeneo mbalimbali kama vile Jiahu, tovuti ya Neolithic nchini China inataja 5700 KK, na jamii za awali za Uhispania za Andean, kama vile tamaduni ya Moche kuanzia Karne ya Pili hadi ya Nane BK.
Katika eneo la Mashariki ya Kati, maandiko na mihuri ya Mesopotamia inaonyesha bia ikinywewa.
Hivyo kuna ushahidi wa bia kutengenezwa kwenye kila bara la dunia ya kale.

Chanzo cha picha, Getty Images
Bia hutengenezwaje?
Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.
Bonyeza hapa kujiunga
Mwisho wa Whatsapp
Kwa kawaida bia hutengenezwa kwa kutumia viungo vinne: maji, shayiri iliyochachushwa, hamira na maua ya kipekee 'hops'.
Maganda ya shayiri yanamenywa kwenye maji ili kuzipa unyevu na kuanzisha mchakato wa kuota.
Kisha, yanachujwa na kukaushwa kwenye tanuru ili kuzuia yasiendelee kuota. Wakati yanapoanza kuota, huzalisha kemikali iitwayo amylase ambayo hubadilisha wanga ulio kwenye maganda kuwa sukari.
Sukari hizi ni muhimu kwa ladha ya bia, na pia humezwa na hamira na baadaye kuchachusha bia ili kutengeneza pombe.
Baada ya kukauka, shayiri hiyo inachomwa kwenye tanuru. Kadri muda wa kuchoma na joto linavyokuwa kubwa, ndivyo rangi ya mwisho inavyokolea na ladha inavyozidi kuwa tayari.
Baada ya hapo, shayiri iliyochachushwa inasagwa na kuunganishwa na maji ya moto ili kutoa sukari. Mchanganyiko huu kisha unachemshwa na maua maalum hops zilizokauka, kisha kupozwa hadi kufikia takribani 20°C (68°F).
Baada ya kupoa, hamira inaongezwa. Hatua ya kuchachusha huchukua wiki kadhaa, kisha bia inachujwa na kujazwa katika chupa.
Kabla ya Mapinduzi ya Viwanda na kuanzishwa matumizi ya tanuru na vyombo vya chuma, hops zilikuwa zikikaushwa juu ya moto, jambo ambalo lilileta ladha ya moshi mkali kwenye bia, anasema Shellhammer hadi baada ya Mapinduzi ya Viwanda na matumizi ya chuma kuwa maarufu.
Shayiri ina harufu na ladha tamu, hivyo hops ni muhimu katika kusaidia kupima ladha tamu na chungu kutoka kwenye hops.
"Ladha ya hops ilikua muhimu kama viungo vingine vya bia, badala ya kuwa shughuli tu ya kitaalamu katika mchakato wa kutengeneza bia."

Chanzo cha picha, Getty Images
Utafiti kuhusu mabadiliko ya tabianchi uliofanywa na Trnka na wenzake ulilenga aina za hops za kiasili.
Kuongezeka kwa joto kunakosababishwa na mabadiliko ya tabianchi kumehamasisha mwanzo wa msimu wa kilimo wa hops za kiasili nchini Ujerumani na Czech kwa siku 13 kati ya mwaka 1970 na 2018, na pia kukomaa kwake kumekuwa mapema kwa siku 20.
Makadirio ya Trnka yanaonyesha kwamba ifikapo mwaka 2050, mavuno ya hops za kiasili yatapungua kati ya 4.1% na 18.4% ikilinganishwa na miaka ya 1989-2018, pamoja na kupungua kwa kiasi cha asidi, kutokana na ongezeko la joto na ukame unaoendelea kuongezeka mara kwa mara.
"Lakini, ikiwa unataka kulima hops zile zile ambazo mababu zetu walilima tangu karne ya 19, au hata kabla, hizi hops za kiasili ambazo zinathaminiwa sana ambazo ni maarufu sana nchini Czech, kuna namna za kubadilisha," anasema Trnka.
Aina mpya za hops zinatengenezwa ili kuwa kukabiliana zaidi na mabadiliko ya tabianchi, anasema Skypeck, lakini kutengeneza aina mpya ya hops kutoka mwanzo hadi uzalishaji kamili kunaweza kuchukua hadi miaka 10.
Kwa mfano, aina mpya inaweza kuonyesha upinzani zaidi kwa joto lakini bado inaweza kuhitaji kiasi sawa cha maji, anasema.
"Watengenezaji bia hutumia mbinu tofauti pia.
Wazalishaji bia nchini Marekani mara nyingi hawatumii aina moja tu ya hops katika bia zao, badala yake hutumia ladha na harufu tofauti ili kuunda upekee.
Kwa upande mwingine, watengenezaji bia wa Kijerumani wanaweza kupata hasara kutumia aina mpya za hops kwa sababu hawataki kubadilisha bia zao ambazo zimekuwa thabiti kwa miaka."

Chanzo cha picha, Getty Images
Christian Ettinger, muasisi wa Hopworks Urban Brewery huko Portland, nchini Marekani anasema kuwa moja ya bia zao za kawaida inaweza kuwa na aina kati ya mbili na tano za hops, jambo linalomuwezesha mtengenezaji huyo kubadilisha utengenezaji kulingana na mabadiliko ya mavuno.
Upungufu wa maji ni moja ya sababu kuu za mavuno duni nchini Marekani, jambo linalosababisha gharama za hops kupanda, anasema Ettinger. "Bia imekuwa kinywaji chenye kileo kinachopendwa zaidi kwa miaka 9,000, na sehemu ya hilo ni upatikaji wake wa bei nafuu.
Ni jukumu letu sisi kama waendelezaji kuhakikisha kuwa bado inapatikana kwa wote."
Ettinger amekuwa akitengeneza bia kwa miaka 30 na katika kipindi hicho ameona jinsi sekta hiyo ilivyobadilika katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kwa kuanzisha mbinu za kilimo endelevu ambayo inahusisha kilimo cha mazao mengine kati ya mimea ya hops ili kudhibiti magugu, kupunguza mmomonyoko wa udongo, na kuboresha afya ya udongo ambayo ni kuongeza nyenzo za kikaboni zenye kaboni nyingi zinazoboresha uwezo wa udongo kuhimili maji.














