Ifahamu bendi hii ya wanawake pekee Tanzania
Bendi ya wanawake huwa ni nadra sana kuskika kutokana na dhana kwamba wanawake hawawezi kushirikiana.
Bahati female Band ni bendi ya kike ya kipekee nchini Tanzania, ambayo shughuli zake zote zinaendeshwa na wanawake kuanzia mpiga ngoma, kinanda na hata waimbaji wote ni wanawake.
Mwanzilishi wa bendi hiyo anaamini kuwa wanawake wakifanya kazi kwa pamoja hufanya mabadiliko kwa muda mfupi.