Aliyenusurika kwenye tukio la kukanyagana asimulia
Watu 20 wamefariki dunia mjini Moshi walipokuwa wakikusanyika katika viwanja vya Majengo kuhudhuria Ibada iliyoongozwa na Mtume Boniface Mwamposa.
Watu hao wamefariki dunia baada ya kukanyagwa na wenzao wakati wakitoka katika lango moja waliloelekezwa kupita ili kukanyaga mafuta ya upako.